Picha ambayo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha muigizaji wa Bongo Movie Chopa Mchopanga
akiwa amevalia jezi ya timu ya Yanga, mkononi akiwa ameshika vidonge
vingi na chupa ya bia, huku ikisemekana kuwa alitaka kujiua kutokana na
kuwa mshabiki mkubwa wa timu ya Yanga ambayo ilifungwa hivi karibuni
pamoja na kuliwa fedha alizokuwa amewekeana dau na star wa Bongo Movie JB.
Soudy Brown alimtafuta Mchopanga
ambae amesema hiyo picha ilitolewa kwenye movie yake mpya iliyotoka
hivi karibuni, inayohusu story za mahaba na haihusiani na mechi ya Yanga
iliyochezwa hivi karibuni, ingawa yeye ni mshabiki mkubwa wa Yanga na
anaipenda lakini hawezi kujiua kwa sababu ya timu hiyo kufungwa
ConversionConversion EmoticonEmoticon