Duru
za kuaminika za ndani ya jeshi la Nigeria zimefichua kuwa, asilimia
kubwa ya silaha za kundi la Boko Haram zinatoka ndani ya jeshi la nchi
hiyo na wala hazitoki kwa mtandao wa al Qaida ambao unatuhumiwa kufanya
vitendo vingi vya kigaidi katika nchi jirani za Chad, Niger, Mali na
Mauritania.
Televisheni
ya lugha ya Kiingereza ya Aljazeera ya Qatar imezinukuu duru hizo za
jeshi la Nigeria ambazo haikuzitaja jina zikisema kuwa, kuna uwezekano
mkubwa sana kwamba baadhi ya maafisa wa kijeshi wa nchi hiyo
wanashirikiana na Boko Haram.
Matamshi
hayo yamekuja baada ya ripota wa televisheni hiyo kuripoti kutoka
Nigeria kwamba, wanamgambo wa Boko Haram leo Jumapili wameanzisha
mashambulizi makubwa dhidi ya mji wa Maiduguri, makao makuu ya jimbo la
Borno pamoja na mji wa Monguno wa jimbo hilo.
Hadi
tunaandaa habari hiyo, mapigano makali yalikuwa yanaendelea katika
viunga vya Maiduguri kati ya jeshi na wanamgambo wa Boko Haram. Jeshi la
Nigeria limekuwa likifanya pia mashambulizi ya anga dhidi ya
wanamgambo hao na kutekeleza pia sheria ya hali ya hatari katika mji
huo.
Kundi
hilo la kitakfiri limeanza operesheni ya kuushambulia mji wa Maiduguri
kutokea katika eneo la Njimtilo. Hivi karibuni pia kundi la Boko Haram
liliripotiwa kufanya mauaji makubwa ya watu katika mji wa Baga, karibu
na mpaka wa Chad baada ya kuuteka mji huo.
cHANZO: kiswahili.irib.ir
ConversionConversion EmoticonEmoticon