.

RIYAMA: NIMEMPITA BABA WATOTO WANGU MIAKA 10


  • Staa mkali wa filamu Bongo, Riyama Ally akiwa na mwanaye aitwaye Fatma.
    Na Imelda Mtema/Amani
    STAA mkali wa filamu za Bongo, Riyama Ally amefunguka kwa kinywa chake kuwa baba aliyezaa naye mtoto wake wa kike aitwaye Fatma, amempita takriban miaka 10.
    Riyama alizungumza hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi kimoja cha TV na kusema kuwa hakuna chochote kinachohusiana na umri katika suala la mapenzi kwa sababu ingekuwa kuna tatizo basi kwa upande wake ingekuwa shida.
    Riyama Ally akiwa na baba watoto wake.
    “ Jamani sidhani kama kuna uhusiano wowote wa umri katika mapenzi, mimi nimempita baba mtoto wangu miaka 10 na hata mpenzi wangu wa sasa naye nimempita hivyohivyo, umri hauna nafasi kabisa kwangu,” alisema Riyama.
Previous
Next Post »