-
Unadhani simu yako ya mkononi ni kichaka kikubwa kinachoweza kuhifadhi siri zako zote?Jibu ni hapana. Kwani teknolojia inamwezesha mtumiaji yeyote kuingilia mawasiliano katika simu yako na kufyonza taarifa mbalimbali kama ujumbe mfupi, barua pepe, simu zinazotoka na kuingia, picha unazopiga au kutumiwa hata video, pia inaweza kubaini eneo alipo mtu.Kwa lugha nyepesi kitendo hiki huitwa udukuzi.Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma anafafanua udukuzi akieleza kuwa ni matumizi ya teknolojia inayowezesha kuingilia mawasiliano ya mtu katika simu au kifaa chochote cha mawasiliano.
Udukuzi wa SerikaliNovemba mwaka jana, Kampuni ya Kimataifa ya Simu za Mkononi ya Vodafone, ilitoa taarifa inayoonyesha kuwa Serikali ya Tanzania imeweka nyaya za siri katika mtandao wa Vodacom na kunasa mawasiliano ya wateja 98,765 kwa mwaka 2013.Katika ripoti hiyo,(Law Disclosure Enforcement), Tanzania inatajwa kuwa ni nchi ya pili duniani miongoni mwa nchi 29 ambazo Vodafone inatoa huduma ikiwa nyuma ya Italia kwa kufuatilia, kuingilia au kunasa mawasiliano ya simu.Italia inashika nafasi ya kwanza kwa mawasiliano 605,601 ya raia wake kufuatiliwa na taasisi za kiusalama za Serikali.Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba alidai kushtushwa na taarifa za Serikali kunak-ili mawasiliano ya simu kwa kutumia nyaya za siri.“Hata mimi imenishtua kidogo kwa sababu sheria za usalama za mawasiliano, kunakili chochote kunafanyika kwa sheria tu,” anasema.Hata hivyo, Makamba anakiri kuwa Serikali kupitia taasisi za usalama hulazimika kuomba taarifa za wateja kwa ajili ya uchunguzi.- Mwananchi
‘Matumizi makubwa ya fedha vyama vya siasa yanatia shaka’
Posted:2015-01-24 05:25:00 UTC+03:00
Wataalamu
wa kilimo huwashauri wakulima kuchagua mbegu bora za kupanda kwenye
udongo mzuri ulio na rutuba, ili zizae na kuleta mavuno yenye faida.
Nao
wanasiasa wanautazama mwaka huu 2015 wa Uchaguzi Mkuu kama shamba
lililo na rutuba, lakini mkulima hana uhakika na mbegu alizoshika
mkononi kwamba ni ipi itampa matokeo mazuri.
Ni
ukweli usiofichika kwamba kwenye miaka ya karibuni, vyama vya siasa
vimekuwa vikitumia fedha nyingi kwenye mikutano yao na ndani na nje,
ili kuhakikisha kuwa mtu anayechaguliwa na chama anakibeba kwa kuzaa
matunda mema ya kupata madaraka, jambo ambalo linatia shaka.
Akiwasilisha
matokeo ya utafiti uitwao ‘Upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ushindani
wa kisiasa’, Profesa Mohabe Nyirabu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
anasema ongezeko la matumizi makubwa ya fedha kwenye vyama vya siasa
linatia shaka.
Anasema
kuwa kwa jumla vyama vya siasa vipo katika wakati mgumu ‘vikihaha’
kutafuta fedha nyingi za kufanyia kampeni na kutafuta wanachama wapya,
lakini huku vikipoteza imani yao mbele ya wananchi kuhusu matumizi ya
fedha.
Profesa
Nyirabu anasema kuwa matumizi ya fedha nyingi kwenye vyama vya siasa
yameongezeka zaidi baada ya kuanzishwa kurejeshwa kwa mfumo wa vyama
vingi nchini.
“Kama
matumizi ya fedha nyingi na utoaji wa rushwa umekithiri katika jamii,
zinatakiwa sera zinazosimamia matumizi ya fedha ndani ya vyama hivyo
ziboreshwe,” anaeleza Profesa Nyirabu.
Msomi
huyo kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma ya Udsm,
anasema katika nchi yenye mfumo wa kidemokrasia, umma huvichangia fedha
vyama kwa sababu kuu tatu.
Sababu
ya kwanza ni kwa ajili ya kuviwezesha vyama hivyo kukua na kusambaza
itikadi na sera zake kwa wanachama wake. Pia, michango ya fedha hukipa
chama uhakika wa kuendelea kuwapo na kukinusuru na ushawishishi
kukisambaratisha. Anataja lengo la tatu la michango hiyo kwa vyama vya
siasa kuwa ni kuviwezesha kusimama kidete dhidi ya ushawishi kutoka
taasisi binafsi na mashirika ya kigeni.
Profesa
huyo anasema kwamba kwa kuwa baadhi ya vyama vya siasa vinaonekana
kutumia fedha nyingi kuliko mapato yanayopatikana, kuna haja ya vyanzo
vya mapato hayo kuwekwa bayana.
“Kuwa
na mapato kwenye vyama vya siasa siyo jambo baya, matokeo ya mara kwa
mara ya rushwa kwenye uchaguzi ni dalili za kuwapo kwa tatizo
linalohusu matumizi ya fedha nyingi kwenye siasa,” anasema Profesa
Nyirabu.
Matokeo ya utafiti huo yanaeleza kuwa
wakati wa mfumo wa chama kimoja cha siasa, mapato kwa ajili ya
kuendesha chama hicho yalitokana na michango kutoka kwa wanachama
ConversionConversion EmoticonEmoticon