.

Hofu mpya kwa watumiaji wa simu za mkononi


  • Unadhani simu yako ya mkononi ni kichaka kikubwa kinachoweza kuhifadhi siri zako zote?

    Jibu ni hapana. Kwani teknolojia inamwezesha mtumiaji yeyote kuingilia mawasiliano katika simu yako na kufyonza taarifa mbalimbali  kama ujumbe mfupi, barua pepe, simu zinazotoka na kuingia, picha unazopiga au kutumiwa hata video, pia inaweza kubaini eneo alipo mtu.

     Kwa lugha nyepesi kitendo hiki huitwa udukuzi.

    Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma anafafanua udukuzi akieleza kuwa ni matumizi ya teknolojia inayowezesha kuingilia mawasiliano ya mtu katika simu au kifaa chochote cha mawasiliano.


    Udukuzi wa Serikali

    Novemba mwaka jana, Kampuni ya Kimataifa ya Simu za Mkononi ya Vodafone, ilitoa taarifa inayoonyesha kuwa Serikali ya Tanzania imeweka nyaya za siri katika mtandao wa Vodacom  na kunasa mawasiliano ya wateja 98,765 kwa mwaka 2013.

    Katika ripoti hiyo,(Law Disclosure Enforcement), Tanzania inatajwa kuwa ni nchi ya pili duniani miongoni mwa  nchi 29 ambazo Vodafone inatoa huduma ikiwa nyuma ya Italia kwa kufuatilia, kuingilia au kunasa mawasiliano ya simu.

    Italia inashika nafasi ya kwanza kwa mawasiliano 605,601 ya raia wake kufuatiliwa na taasisi za kiusalama za Serikali.

    Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba alidai kushtushwa na taarifa za Serikali kunak-ili mawasiliano ya simu kwa kutumia nyaya za siri.

     “Hata mimi imenishtua kidogo kwa sababu sheria za usalama za mawasiliano, kunakili chochote kunafanyika kwa sheria tu,” anasema.

    Hata hivyo, Makamba anakiri kuwa Serikali kupitia taasisi za usalama hulazimika kuomba taarifa za wateja kwa ajili ya uchunguzi.
    - Mwananchi

‘Matumizi makubwa ya fedha vyama vya siasa yanatia shaka’

Posted:2015-01-24 05:25:00 UTC+03:00
Wataalamu wa kilimo huwashauri wakulima kuchagua mbegu bora za kupanda kwenye udongo mzuri ulio na rutuba, ili zizae na kuleta mavuno yenye faida.
Nao wanasiasa wanautazama mwaka huu 2015 wa Uchaguzi Mkuu kama shamba lililo na rutuba, lakini mkulima hana uhakika na mbegu alizoshika mkononi kwamba ni ipi itampa matokeo mazuri.
Ni ukweli usiofichika kwamba kwenye miaka ya karibuni, vyama vya siasa vimekuwa vikitumia fedha nyingi kwenye mikutano yao na ndani na nje, ili kuhakikisha kuwa mtu anayechaguliwa na chama anakibeba kwa kuzaa matunda mema ya kupata madaraka, jambo ambalo linatia shaka.
Akiwasilisha matokeo ya utafiti uitwao ‘Upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ushindani wa kisiasa’, Profesa Mohabe Nyirabu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anasema ongezeko la matumizi makubwa ya fedha kwenye vyama vya siasa linatia shaka.
Anasema kuwa kwa jumla vyama vya siasa vipo katika wakati mgumu ‘vikihaha’ kutafuta fedha nyingi za kufanyia kampeni na kutafuta wanachama wapya, lakini huku vikipoteza imani yao mbele ya wananchi kuhusu matumizi ya fedha.
Profesa Nyirabu anasema kuwa matumizi ya fedha nyingi kwenye vyama vya siasa yameongezeka zaidi baada ya kuanzishwa kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini.
“Kama matumizi ya fedha nyingi na utoaji wa rushwa umekithiri katika jamii, zinatakiwa sera zinazosimamia matumizi ya fedha ndani ya vyama hivyo ziboreshwe,” anaeleza Profesa Nyirabu.
Msomi huyo kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa na Uongozi wa Umma ya Udsm, anasema katika nchi yenye mfumo wa kidemokrasia, umma huvichangia fedha vyama kwa sababu kuu tatu.
Sababu ya kwanza ni kwa ajili ya kuviwezesha vyama hivyo kukua na kusambaza itikadi na sera zake kwa wanachama wake. Pia, michango ya fedha hukipa chama uhakika wa kuendelea kuwapo na kukinusuru na ushawishishi kukisambaratisha. Anataja lengo la tatu la michango hiyo kwa vyama vya siasa kuwa ni kuviwezesha kusimama kidete dhidi ya ushawishi kutoka taasisi binafsi na mashirika ya kigeni.
Profesa huyo anasema kwamba kwa kuwa baadhi ya vyama vya siasa vinaonekana kutumia fedha nyingi kuliko mapato yanayopatikana, kuna haja ya vyanzo vya mapato hayo kuwekwa bayana.
“Kuwa na mapato kwenye vyama vya siasa siyo jambo baya, matokeo ya mara kwa mara ya rushwa kwenye uchaguzi ni dalili za kuwapo kwa tatizo linalohusu matumizi ya fedha nyingi kwenye siasa,” anasema Profesa Nyirabu.
Matokeo ya utafiti huo yanaeleza kuwa wakati wa mfumo wa chama kimoja cha siasa, mapato kwa ajili ya kuendesha chama hicho yalitokana na michango kutoka kwa wanachama
Previous
Next Post »