- Ikiwa na nyota wake Cristiano Ronaldo na Gareth Bale, Real Madrid imechukua kipigo cha aibu 4-0 kutoka kwa watani wao wakubwa Atletico Madrid.Hii ni mara ya kwanza ndani ya miaka 64 kwa Real Madrid kufungwa mara tatu mfululizo kwenye uwanja wa wapinzani wao hao wa jiji la Madrid, lakini kipigo hiki kilikuwa cha aibu zaidi - klabu hiyo tajiri ilifunikwa vibaya kuanzia filimbi ya kwanza hadi mwisho wa mchezo.Washambuliaji wa Real Madrid wenye thamani ya pauni milioni 250 Bale, Ronaldo na Karim Benzema walifanikiwa kupiga shuti moja tu katika kipindi cha kwanza kilichotawaliwa na Atletico Madrid ambao walifunga mara mbili kupitia kwa Tiago na Saul.Magoli mengine ya Atletico Madrid katika mchezo huo wa La Liga, yalifungwa na Greizmann na Mandzukic.Atletico Madrid (4-4-2): Moya; Juanfran, Miranda, Godin, Siqueira; Tiago, Koke (Saul 10 [Garcia 71]), Gabi, Turan; Griezmann (Torres 77), Mandzukic.
.
Uncategories
REAL MADRID YASHIKWA PABAYA LA LIGA, YAPIGWA 4-0 NA ATLETICO MADRID - Bale, Ronaldo na Benzema watiwa mfukoni
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
ConversionConversion EmoticonEmoticon